JE UNATAKA KUWA NA FOLLOWERS WENGI INSTAGRAM,BASI FUATA MAELEKEZO HAYA

Instagram Changes Terms Of Service, Stirs Anger Among Users
1. Caption
Beyoncé huweka picha nzuri sana kwenye Instagram lakini kama angekuwa anaziwekea caption, zingependeza zaidi. Hata hivyo huyo ni staa tayari hivyo hili linaweza lisiwe na madhara sana kwake. Caption huzipa uhai picha zako na kama utaziandika kwa ubunifu, ni rahisi kupata likes na hata follows nyingi.
2. Hashtags
Hashtags zina kazi zake maalum. Hashtags ni njia nzuri za kuvuta traffic kwenye picha zako lakini zifanye zihusiane na picha – kwakuwa zikiwa nyingi zinaweza kuwakera followers wako.
3. Selfies
Selfies ni nzuri kupost hapa na pale. Ukiziweka nyingi na tena ambazo hazina mvuto unaweza kuishia kuchezea unfollow za kutosha kwa kuijaza tu timeline.
4. Weka picha zenye ubora
Siku zote weka picha nzuri zaidi. Chagua picha kali.
5. Zikusanye
Badala ya kumwaga picha kumi zenye muonekano unaofanana au eneo moja, ziunganishe na upost kama picha moja.
6. Repost
Kuna picha nzuri unayoweza kuiona kwenye akaunti ya mtu mwingine. Irepost ili watu wanaokufollow waweze kuiona pia.
7. Like!
Usiwe mtu wa kupost tu picha na kuondoka. Chukua muda wa kulike pia picha za wengine au kucomment pale unapoguswa.
8. Screenshots Whatsapp
Unaweza ukawa umechat na mtu kwenye whatsapp na mazungumzo hayo kuwa na kitu cha kufurahisha. Unaweza ukaipost ilimradi tu isiwe na ujumbe wenye utata.
9. Chakula, wanyama, watoto
Tunaona watu wengi wakipost picha wakiwa mezani wakila chakula kitamu, kupost picha za wanyama wanaowafuga au za familia zao. Kikubwa ni kuweka kwa kiwango.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post