1. Caption
Beyoncé
huweka picha nzuri sana kwenye Instagram lakini kama angekuwa
anaziwekea caption, zingependeza zaidi. Hata hivyo huyo ni staa tayari
hivyo hili linaweza lisiwe na madhara sana kwake. Caption huzipa uhai
picha zako na kama utaziandika kwa ubunifu, ni rahisi kupata likes na
hata follows nyingi.
2. Hashtags
Hashtags
zina kazi zake maalum. Hashtags ni njia nzuri za kuvuta traffic kwenye
picha zako lakini zifanye zihusiane na picha – kwakuwa zikiwa nyingi
zinaweza kuwakera followers wako.
3. Selfies
Selfies
ni nzuri kupost hapa na pale. Ukiziweka nyingi na tena ambazo hazina
mvuto unaweza kuishia kuchezea unfollow za kutosha kwa kuijaza tu
timeline.
4. Weka picha zenye ubora
Siku zote weka picha nzuri zaidi. Chagua picha kali.
5. Zikusanye
Badala ya kumwaga picha kumi zenye muonekano unaofanana au eneo moja, ziunganishe na upost kama picha moja.
6. Repost
Kuna picha nzuri unayoweza kuiona kwenye akaunti ya mtu mwingine. Irepost ili watu wanaokufollow waweze kuiona pia.
7. Like!
Usiwe mtu wa kupost tu picha na kuondoka. Chukua muda wa kulike pia picha za wengine au kucomment pale unapoguswa.
8. Screenshots Whatsapp
Unaweza
ukawa umechat na mtu kwenye whatsapp na mazungumzo hayo kuwa na kitu
cha kufurahisha. Unaweza ukaipost ilimradi tu isiwe na ujumbe wenye
utata.
9. Chakula, wanyama, watoto
Tunaona
watu wengi wakipost picha wakiwa mezani wakila chakula kitamu, kupost
picha za wanyama wanaowafuga au za familia zao. Kikubwa ni kuweka kwa
kiwango.