KUHUSU MTOTO ALBINO KUTEKWA HUKU WAZAZI WAKISHUHUDIA HUKO GEITA

NB-PICHA HAIHUSIANI NA HABARI HAPA CHINI

Mtoto mwenye ulemavu wa ngozi, albino ametekwa katika wilaya ya Chato mkoa wa Geita.
Polisi wameeleza kuwa mtoto huyo aliyetajwa kwa jina la Yohana Bahati mwenye umri wa mwaka mmoja alitekwa nyumbani kwao na watu wasiojulikana jana usiku.
Kwa mujibu wa taarifa za mwandishi kutoka eneo hilo Renatus Masuguliko, polisi wamefika eneo la tukio na kuanza msako mkali dhidi ya watu wanaotuhumiwa kufanya kitendo hicho.
Habari zinasema watu waliokuwa na silaha za jadi waliwaweka chini ya ulinzi Bahati Misalaba na mkewe ambao ni wazazi wa mtoto albino ambaye walimteka na kutoweka naye.
Familia hii pia ina watoto wengine wawili wenye ulemavu wa ngozi, Tabu Bahati mwenye umri wa miaka miwili na Shida Bahati mwenye miaka kumi na mmoja ambao walinusurika kuchukuliwa na watu hao kwa sababu wakati unyama huo ukitendeka nyumbani kwao hawakuwepo walikwenda kucheza kwa majirani zao.
Mama wa mtoto huyo alijeruhiwa vibaya wakati akimpigania mtoto wake asichukuliwe na watu hao.
Matukio ya kuwaua na kuchukua viungo vya albino yaliyasambaa katika mikoa ya kanda ya Ziwa kutokana na imani za kishirikina kuwa viungo vya watu hao vingeweza kuwapatia utajiri na mafanikio mengine katika maisha yao, jambo ambalo ni upuuzi mtupu.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post