Laana!! NJEMBA YAOA MTOTO WA MIAKA 10, BIBI WA MTOTO ABARIKI NDOA NA MASHAHIDI WATATU


Mwandishi wa habari na mtangazaji wa Radio Rasi FM ya Dodoma Oscar Kiwanga Kahuka akizungumza na bibi anayedaiwa kubariki ndoa ya mtoto mdogo huko Dodoma

Mwanaume mmoja kwa jina la Joshua Mnhamba mwenye umri wa miaka 27 Mkazi wa Ibihwa wilayani Bahi mkoani Dodoma anashikiliwa na Jeshi la polisi kwa kuishi na mtoto mwenye umri wa miaka kumi kama mke wake baada ya moto huyo kuozeshwa na bibi yake.

Mwanaume huyo alifunga ndoa na Neema Stephano mwenye umri wa miaka 10 mnamo Januaryi 27 mwaka huu huko kijiji cha Ibihwa kwa lazima, ambapo bibi wa msichana huyo Bibi Ntolwa Malambu Mpondo akishuhudia tukio hilo  na mashahidi wengine watatu.

Hata hivyo alipoulizwa bibi yake amekana kuwa yeye hahusiki na tukio hilo huku akiwatupia mzigo huo wazazi wa mtoto huyo kwa kudai wao ndiyo waliomuoza na yeye hana mamlaka ya kuingilia familia ya watu.

Kaimu mtendaji wa kijiji cha ibihwa Noro Said Noro amelaani kitendo hicho huku akiwataka wanakikiji kutoa taarifa katika matukio yote ya namna hiyo ili wahusika waweze kuchukuliwa hatua stahiki.

Tayari jeshi la polisi linamshikilia mwanamme huyo kwa mahojiano zaidi ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yake.

Na Josephine Charles Malunde1 blog- Dodoma

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post