Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini Inspekta Jenerali (IGP) Ernest Mangu |
Mwanamke aitwaye Mary Kashindye(45)
mkazi wa kijiji na kata ya Mangolo tarafa ya Kahama mjini wilayani Kahama mkoani Shinyanga ameuawa kwa kupigwa risasi
tumboni na watu wasiofahamika akiwa nyumbani kwake.
Kaimu Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga SS Longinus Tibishubwamu amesema mwanamke huyo aliuawa akiwa
nyumbani kwake jana.
Amesema chanzo cha tukio hilo inasadikiwa
kuwa ni ugomvi wa kiwanja baina yake na Jumanne Maige ambaye ndiyo anatiliwa
mashaka na mwenzake Abdallah Kashindye.
Amesema jeshi la polisi linaendelea na msako wa kuwakamata
watuhumiwa wa tukio hilo huku akitoa wito kwa wananchi kutoa ushirikiano
utakaofanikisha kukamatwa kwa watuhumiwa.
Tukio hilo linakuja siku moja tu baada ya miili ya watu watatu akiwemo mganga wa kienyeji kukutwa imeharibika vibaya ndani ya nyumba kutokanana kilichodaiwa kuwa waliuawa kwa kukatwa mapanga na watu wasiofahamika katika kijiji cha Bugogo kata ya Mwamala wilaya ya Shinyanga
Na Kadama Malunde-Shinyanga