MFANYAKAZI WA GAZETI LA MWANANCHI APIGWA RISASI

Mfanyakazi wa Kampuni ya Mwananchi Communications, Patrick Pella.
Mfanyakazi  wa Kampuni ya Mwananchi Communications, Patrick Pella amevamiwa na majambazi wenye silaha na kupigwa risasi, kujeruhiwa na kisha kuporwa fedha zake leo mchana  maeneo ya Tabata-Relini jijini Dar es salaam
Kwa mujibu wa chanzo chetu, Pella anadaiwa kuporwa kiasi cha Sh. Mil 2 alizokuwa nazo akiwa ametoka kuzichukua kwenye mashine ya kutolea fedha (ATM) Tawi la NMB liliyopo jirani na Azam TV, Barabara ya Mandela.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Ilala, Mary Nzuki.
Mtandao huu ulimtafuta Kamanda wa Polisi mkoa wa Ilala, Mary Nzuki kuelezea zaidi tukio hilo, lakini simu yake iliita bila kupokelewa.
 
via>> http://www.williammalecela.com

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post