Vitendo vya
kikatili na unyanyasaji wa Wanawake na watoto vinaendelea kushika kasi licha ya
Serikali na mashirika mbalimbali ya haki za Binadamu kupiga vita vitendo hivyo
kwa nguvu visijiokeze tena.
Hali hiyo
imejitokeza katika kijiji cha Kasaka, Kata ya Nyaruyoba Wilaya ya Kibondo
mkoani Kigoma baada ya Baba mzazi aliyefahamika kwa jina la Sindotuma Nyamubi,
kumchoma moto na kumuunguza vibaya sehemu za mdomoni wake, mtoto wake wa miaka
saba akimtuhumu kudokoa maharage yaliyotakiwa kutumika kama mboga kwa ajili ya
kulia chakula.
Afisa
Mtendaji wa kijiji hicho Bwa Felix Cosmas amesema kuwa mtoto huyo alibainika
kuwa amefanyiwa kitendo hicho baada ya majirani kutomuoana akicheza na wenzake
kwa muda wa siku tatu kama ilivyokuwa imezoeleka, ndipo walipogundua alikuwa
amefichwa ndani ya nyumba na kugundua tatizo hilo na kutoa taarifa hatua
iliyofanikisha mzazi huyo kukamatwa na kufikishwa Polisi.
Naye Afisa
Ustawi wa Jamii wilaya ya Kibondo,Bi Sofia Gwamagobe amesema kuwa ni vizuri
wazazi na walezi kutambua na kujali hali za watoto na sambamba na jamii pia
kuendelea kufichua na kutoa taarifa katika vyombo husika ili kuweza kuokoa
maisha watu wanaofanyiwa mambo kama hayo kama wamejeruhika kuwapatia matibabu
kabla hawajapata madhara makubwa
Hata hivyo
Mkuu wa Jeshi la Polisi wilayani Kibondo, amekili kuwepo kwa tukio hilo, na
kumtaja aliyejeruhiwa vibaya kuwa ni Shukuru Sindotuma na amesema baada ya mtuhumiwa
huyo kufikishwa kituoni hapo, amekubali kuwa alimchoma moto mtoto wake kwa kosa
la kula maharage bila ruhusa yake
Aidha Baba
huyo aliyefanya kitendo hicho ambacho si cha uungwana kwa Mzazi/Mlezi kikufanya
kwa Mtoto wake , amehukumiwa kifungo cha miaka mitano Gerezani baada kukutwa na
hatia ya Kumfanyia ukatili mtoto wake kwa Kumuunguza mdomoni na kumsababishia
maumivu makali .
Nao baadhi
wazazi wakazi wa kibondo wamelaani kitendo hicho kilichofanywa na mzazi mwenzao
kuwa ni kitendo cha kikatili na kuwataka wanajamii kuacha kutumia hasira kali
kwa watoto wadogo
Mtoto huyo
Shukuru Sindotuma alikuwa anaishi na baba yake ,mdogo wake mmoja huku Wazazi
wao wakiwa wametengana na baada ya kupata Matibabu katika Hopitali ya wilaya ya
Kibondo ,amesafirishwa kwenda wilayani Kasulu mkoani Kigoma kwenda kuishi na
Mama yake mzazi.