Utafiti! WANAWAKE WANNE KATI YA WATANO HAWAOGI KILA SIKU,WENGINE HAWALALI KWA SABABU YA UREMBO WAO

Wanawake wanne kati ya watano wamekiri wazi kuwa huwa hawaogi kila siku,na wengine wanadai kuwa wanaweza kukaa kwa siku tatu bila miili yao kukutana na maji.


Utafiti uliofanywa nchini Uingereza kukagua ngozi za wanawake 2,021 wenye umri wa kati ya miaka 18 hadi 50 umegundua kuwa mbili ya tatu ya wanawake wana tabia ya kutoosha nyuso zao zenye poda kabla ya kulala na moja ya nane ya wanawake pia huwa hawana utamaduni wa kupiga mswaki kabla ya kulala.

Linapokuja suala la kuoga asubuhi sasa,ni asilimia ishirini na moja tu ya wanawake ambao hutenga muda wa kuoga asubuhi kila siku,na asilimia thelathini na tatu ya wanawake huishi kwa siku tatu bila ya kukutana na maji mwillini mwao.

Jambo la kushangaza mmoja kati ya wanawake watatu huthubutu kukaa kwa siku tatu bila ya kuosha nyuso zao pia, kama utashangaa juu ya miili isiyooshwa kwa siku tatu.

Pamoja na kwamba wataalamu wa masuala ya fya na usafi wa kawaida wa mwili, asilimia hamsini na saba ya wanawake wa Uingereza wanakiri kutumia karatasi laini zenye maji maji kujifuta mwilini kabla ya kulala.

Utafiti uliofanywa uliwafikia wanawake elfu mbili,inaelezwa kuwa asilimia tisini na mbili wamesema wazi kuwa wanaelewa umuhimu wa utunzaji ngozi,lakini mtindo wa maisha huwanyima usingizi na ukosefu wa maji mwilini na hivyo kujiletea madhara kiafya na hasa ngozi zao.

HUWA UNAOGA MARA NGAPI?
Kila siku? Baada ya siku moja? Mara mbili kwa wiki,mara moja kwa mwezi? Iwe nataka ama lah,utafiti ukaeleza kuwa asilimia themanini na tisa ya wanawake wanajitetea kuwa wangependa sana kusafisha miili yao lakini uchovu wa asubuhi na jioni ndio sababu ya kutooga.

Mmiliki wa kampuni ya afya ya Flint + Flint Maxine Flint anasema kwamba anaelewa kuwa wanaojitetea wanadanganya, na kutooga hasa asubuhi haikubaliki kijamii, kwa watu wanaotuzunguuka na sio afya.

Anasema tunazungumzia dakika chache unazitumia kuoga kwa siku nzima,inaeleweka kuwa maisha ya sasa ni haraka haraka lakini kila mmoja pale alipo sio kweli kwamba hata muda wa kuoga tunaukosa, hatujatingwa kihiivyo.

Kwa muujibu wa taratibu za afya Maxine anasema ni vyema kusafisha nyuso zetu kila subuhi na kuukanda kwa joto ili kuchelewesha uzee usoni.Zaidi ya hayo ,idadi kubwa ya wanawake wanaelewa umuhimu wa utunzaji ngozi lakini bado hawazitunzi.
via>>BBC

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post