Wabongo Bwana !! SUTI YA MHESHIMIWA STEVEN WASSIRA YAZUA GUMZO MTANDAONI KISA KUKOSEWA KUFUNGWA VIFUNGO!!

 
Suti  ya  Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Mh Steven Wassira  imegeuka  gumzo  mtandaoni baada  ya  kukosewa  kufungwa  vifungo  vyake.....


Wassira  alionekana  ndani  ya  vazi  hilo wakati  wa   Sherehe za Utume zilizoandaliwa na kanisa la Waadventista Wasabato (SDA) na kujumuisha nchi zingine 11 za Afrika Mashariki na Kati.

Sherehe  hizo  zilizofanyika  juzi uwanja wa taifa  Dar  es salaam zilihudhuriwa  na kiongozi wa Kanisa la Waadventista Wasabato (SDA) duniani, Askofu Ted Wilson ambapo mgeni rasmi  wa  sherehe  hizo  alikuwa  ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal
 

Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Mh Steven Wassira (wa pili toka kushoto) akiwa katika  picha ya pamoja  na  kiongozi wa Kanisa la Waadventista Wasabato (SDA) duniani, Askofu Ted Wilson( wa  nne toka kushoto) wakati wa sherehe za utume wa kanisa  hilo.
Chanzo-Kibonajoro.com

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post