WACHIMBAJI WADOGO WA MADINI SHINYANGA WALILIA MSAADA WA VIFAA VYA KUFANYIA KAZI


Wachimbaji wadogo wa madini aina ya Dhahabu, walioko katika eneo la Ishinabulandi katika manispaa ya Shinyanga wameiomba serikali kutoa msaada wa vifaa kwa ajili ya shughuli za uchimbaji na uchenjuaji wa madini hayo pamoja na mikopo yenye riba nafuu ili kuboresha uzalishaji na kukuza kipato cha wananchi na taifa kwa ujumla.

Wito huo umetolewa na mkurugenzi wa kampuni ya uchimbaji madini ya dhahabu ya shinyanga Best,Bw.Kashi Salula ambapo amesema serikali imekuwa ikiwaahidi mikopo lakini haifawafikii walengwa hivyo kujikuta wakiendelea kuchimba kwa kutumia dhana zisizokikuwa na tija katika uzalishaji wa dhahabu.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post