BAADA YA SIMBA SC KUIBAMIZA YANGA 1 -O,VITUKO VYATAWALA MTANDAONI,CHEKA UNENEPE SASA




Mchezaji mganda alieleta vuta nikuvute kati ya Klabu Vigogo Nchini baada ya kuhama kwenda nyingine kwa mizengwe mikubwa, Emmanuel Okwi, Leo hii alileta raha kubwa kwa Simba baada ya kufunga Bao pekee na la ushindi walipoilaza Yanga Bao 1-0 kwenye Mechi ya Ligi  Kuu Vodacom.
Bao hilo la Okwi lilifungwa Dakika ya 53 na kuipandisha Simba hadi Nafasi ya 3 wakiwa na Pointi 26 kwa Mechi 17 na juu yao wapo Mabingwa Watetezi Azam FC wenye Pointi 30 kwa Mechi 16 na Yanga bado wapo kileleni wakiwa na Pointi 31 kwa Mechi 16.
Yanga walimaliza Mechi hii wakibaki Mtu 10 baada ya Mchezaji wao Haruna Niyonzima kutolewa nje kwa Kadi Nyekundu karibuni na mwisho.
MATOKEO- Mechi zilizopita:
Jumamosi Machi 7
Coastal Union 2 Kagera Sugar 2  
JKT Ruvu 0 Azam FC 1

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
أحدث أقدم