Duh!! BABA AMNG'ATA SIKIO MTOTO WAKE WAKATI AKICHAPANA MAKONDE NA MKEWE

Fighting
Mwanaume mmoja Nigeria Udeme Inim amekamatwa kwa madai ya kumshambulia na kumng’ata sikio mtoto wake wa kiume wakati akiamulia ugomvi kati yake na mke wake nyumbani kwao mtaa wa Asaka, Nigeria.


Kulitokea hali ya kutokuelewana kati ya wawili hao, Inim alianza kumpiga mke wake ndipo kijana huyo Christopher Bassey alipoingilia kwa lengo na kumwokoa mama yake lakini baba yake alipatwa hasira na kumng’ata sikio na kulikata.
Father-Bits-Off-Son’s-Ear-For-Trying-To-Stop-Him-From-Beating-His-Mother
Bassey alipelekwa Hospitali ya jirani lakini madaktari hawakufanikiwa kurudishia sikio hilo, mwanaume huyo alikamatwa na kushtakiwa kwa kosa la kushambulia  na kuwekwa jela  huku dhamana yake ikiwa ni Naira 20,000.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
أحدث أقدم