HILI NDIYO SHIMO LILILOSABABISHA AJALI HUKO IRINGA, VIFO VYAONGEZEKA SASA NI 50


Shimo hili katikati ya barabara ndilo linasadikika kuwa chanzo cha ajali iliyoua watu 43 na zaidi ya 20 kujeruhiwa, katika eneo la Changarawe Mafinga Iringa.

Idadi ya Vifo katika ajali iliyotokea jana mjini Mafinga Mkoani Iringa imeongezeka na kufikia watu 50 baada ya mtu mmoja kufariki dunia usiku wa kuamkia leo na miili mingine saba ambayo jana haikuhesabiwa, kugundulika mchana wa leo.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Iringa Kamishna msaidizi wa Polisi Ramadahani Mungi amesema kuwa miili hiyo saba iliingizwa katika majokofu moja kwa moja kutoka katika eneo la ajali, hali iliyosababisha isihesabiwe huku akitaja majeruhi kuwa ni 22 na wawili kati yao wakiwa katika hali mbaya.

Katika hatua nyingine Mwenyekiti wa chama cha NCCR Mageuzi James Mbatia ameitaka serikali kuchukua hatua kwa kila aliyehusika na kutokea kwa ajali hiyo, huku akitaka ufanyike uchunguzi wa kina ikiwa ni pamoja na kuchukua hatua za kutoruhusu malori kusafirisha mizigo katika barabara moja na mabasi ya abiria

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post