KUHUSU PADRE FEKI ALIYEKAMATWA HUKO MOROGORO

Jeshi la polisi mkoani morogoro linamshikilia mtu mmoja  Joseph Asenga  mwenye umri wa miaka 47 kwa tuhuma za kujifanya kuwa ni Padre wa kanisa katoliki na hata kuendesha ibada.


Taarifa zilizothibitishwa na kamanda wa polisi mkoa wa morogoro,Leonard Paulo, zimebainisha mtuhumiwa  huyo kutiwa mbaroni katika maeneo ya modeko katika kanisa katoliki la Mt.Maria ambapo anadaiwa kuwahi kufika kanisani hapo kati ya Mei na Juni mwaka jana,kabla ya kurudia tena hivi karibuni, akijitambulisha alikuwa  padri  kwa kutoa vitambulisho feki  akisema ametokea jimbo la NEW YORK nchini marekani na alikuja nchini kwa mapumziko na katika upekuzi amekutwa na majoho saba ya kipadri.
Katibu wa kanisa katoliki, jimbo katoliki la morogoro,Padre Lutsfud Makseyo,amesema amelaani tukio hilo  na kwamba limewasikitisha na kuwahuzunisha kama kanisa,na kutoa wito kwa wananchi kushirikiana na vyombo vya dola kuwafichua watu wote wanaofanya vitendo vya kitapeli kwa kujihusisha na uongozi wa kiimani.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post