Maajabu ya Mungu!! MTOTO ATUMBUKIA KWENYE MTO ULIOFURIKA MAJI KWA SAA 14,AKUTWA AKIWA HAI


Je ushasikia kuwa watoto ni malaika ?


Amini usiamini mtoto wa kike alipatikana hai zaidi ya saa 14 baada ya gari alimokuwa kutumbukia ndani ya mto uliofurika huko Utah marekani.

Kitoto hicho chenye umri wa mwaka mmoja na nusu kilipatikana na wavuvi kinaning'inia ndani ya gari hilo lililokuwa limepinduka ndani ya mto.

Polisi wanasema kuwa mtoto huyo alipatikana akiwa ndani ya kiti cha watoto .

Alikimbizwa hospitalini katika mji wa Salt Lake City, ambapo hali yake inasemekana kuwa imeimarika maradufu.

Mamake mtoto huyo Lynn Groesbeck mwenye umri wa miaka 25 alipatikana ameaga dunia katika kiti cha dereva.

wachunguzi wanasema kuwa mamake mtoto huyo huenda aligonga vizuizi vya barabarani na kutumbukia ndani ya mto Spanish Fork usiku wa kuamkia Jumamosi.

Mvuvi mmoja aliwaarifu polisi baada ya kuona kitoto kikielea ndani ya gari lililopinduka .

Askari watatu na zimamoto wanne walioingia ndani ya maji hayo baridi walilazimika kutibiwa hospitalini baada ya mwili wao kuganda katika operesheni hiyo.
Via>>BBC

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post