MWANAMKE APIGWA MAWE AKITUHUMIWA KUWA NA UHUSIANO WA KIMAPENZI NA MME WA MTU SHINYANGA

Muonekano wa mwanamke huyo sehemu aliyopigwa jiwe

Hekaheka ya leo inatokea Ngokolo mjini Shinyanga, inahusu mwanamke aliyepigwa na jiwe kichwani na kujeruhiwa kwenye sikio kwa kutuhumiwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mume wa mtu.

Inaelezwa kuwa mume na mke walishirikiana kumpiga mwanamke huyo hali ambayo imezua gumzo mtaani kwani ni jambo la kushangaza kuona mume anayetuhumiwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanamke mwingine kushirikiana na mke wake kutembeza kichapo.

Mwanamke huyo aliyepigwa amesema kuwa alitoka kumsindikiza mgeni wake wakati anarudi akapata lift ya pikipiki lakini ghafla alishangaa kupigwa jiwe na watu anaowafahamu ambao ni mtu na mke wake wakazi wa Ngokolo.

Mwanamke huyo amesema baada ya kupigwa walisimama ili kuwauliza kwa nini wampige jiwe lakini waliwakimbia, wakaenda mpaka nyumbani kwa watu hao, lakini hakuweza kuongea nao kwa kuwa walijifungia mlango ndani.

Mwanamke anayetuhumiwa kumpiga jiwe amesema sio kweli kwamba alimpiga jiwe mwanamke huyo na wala hakuwepo kwenye ugomvi huo kwa kuwa yeye alikuwa amelala hivyo hajui chochote.

Mmoja ya mashuhuda wa tukio hilo wanasema ni kweli waliomuona mwanaume na mke wake waliorusha mawe na baada ya kurusha mawe hayo walikimbia kwenda kujifungia ndani ya nyumba yao.
SIKILIZA HAPA CHINI

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
أحدث أقدم