ANGALIA PICHA- RAIS KIKWETE AWATEMBELEA WAHANGA WA MVUA YA MAWE HUKO MWAKATA-KAHAMA

Rais Kikwete akisalimiana na kamati ya ulinzi na usalama mkoa wa Shinyanga baada ya kuwasili mjini Kahama katika uwanja wa ndege wa Buzwagi kwa ajili ya ziara yake kuwatembelea wahanga wa mvua ilionyesha Mwakata Kahama na kuua watu wengi.

Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Jakaya Kikwete leo amewatembelea na kuwafariji wahanga wa mvua ya mawe iliyoambatana upepo iliyoua watu zaidi ya 40 katika kijiji cha Mwakata wilayani Kahama mkoani Shinyanga hivi karibuni-picha zote na Marco Maduhu- Malunde1 blog Kahama
Rais Kikwete akizungumza na baadhi wa wahanga wa mvua.
 Akiwa Mwakata Rais Kikwete amesema serikali inatafuta pesa kwa ajili ya ujenzi wa nyumba 403 kwa ajili ya waathirika wa mvua hiyo na kuahidi kuwapatia chakula wahanga wa mvua hiyo.


 Rais Kikwete akisalimiana na kamati ya ulinzi na usalama mkoa wa Shinyanga baada ya kuwasili mjini Kahama katika uwanja wa ndege wa Buzwagi kwa ajili ya ziara yake kuwatembelea wahanga wa mvua ilinyosha Mwakata Kahama na kuua watu wengi

 Rais Kiwete baada ya kuwasili wilayani Kahama leo
 Rais Kikwete akisalimiana na viongozi wa CCM
 
 Mkuu wa wilaya ya Kahama Benson Mpesya akimwongoza mheshimiwa Rais kuwaona wahanga wa mvua katika kijiji cha Mwakata Kahama


 Rais Kikwete akiwapa mkono wa pole wahanga wa mvua


 Rais Kikwete akiendelea kuwapa pole wakazi wa Mwakata
 
Rais Kikwete akiwa katika makazi ya muda ya wakazi wa Mwakata katika shule ya msingi Mwakata
Rais Kikwete akiwapa mkono wa pole baadhi ya wahanga hao.




Rais Kikwete amesema nyumba hizo zitajengwa na JKT ndani ya siku 90 ambapo wanajeshi watalipwa na serikali-picha na Marco Maduhu- Malunde1 blog Kahama
 
Rais Kikwete pia alihutubia wakazi wa Mwakata
Picha Zote na Marco Maduhu- Malunde1 blog Kahama

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post