SHUHUDIA TUKIO LA AINA YAKE LILILOFANYWA NA CHADEMA LEO KWENYE KITUO CHA ALBINO BUHANGIJA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI

 Baraza la wanawake Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema wilaya ya Shinyanga mjini( BAWACHA) wakiandamana kuelekea kwenye kituo cha kulelea watoto wenye ulemavu wa ngozi (Albino) cha Buhangija mjini Shinyanga wakati wa maadhimisho ya siku ya wanawake duniani,ambapo baraza hilo waliamua kuandamana kupinga vitendo vya mauaji ya albino nchini
-picha na Marco Maduhu-Malunde1 blog

Mwenyekiti wa Bawacha wilaya ya Shinyanga mjini Zenna Gulaam akiongoza maandamano hayo leo asubuhi wakitokea kwenye ofisi za Chadema wilaya ya Shinyanga-picha na Marco Maduhu-Malunde1 blog

 Maandamano ya amani kuelekea Buhangija yakiendelea-picha na Marco Maduhu-Malunde1 blog
 Wakisubiri taratibu za kisheria zifuatwe ili kuingia ndani ya kituo cha watoto albino kutokana na ulinzi mkali uliopo katika eneo hilo,hatimaye wakaruhusiwa kuingia,wakiwa wamebeba msaada wa  chakula ,mchele kilo 100 na  sabuni za kufulia-picha na Marco Maduhu-Malunde1 blog
 Mjasiriamali aliyekuwa ameambatana na akina mama wa BAWACHA,akiwa amebeba vyakula kwa ajili ya watoto hao-picha na Marco Maduhu-Malunde1 blog
 Akina mama wa BAWACHA wakikabidhi msaada wa chakula katika kituo cha Buhangija ambacho sasa kinakabiliwa na uhaba wa chakula na malazi kutokana na idadi ya watoto hao kuzidi kuongezeka kila kukicha wakihofia kuuawa hivyo kukimbilia kituoni hapo kwa ajili ya kunusuru maisha yao-picha na Marco Maduhu-Malunde1 blog

Mwenyekiti wa Bawacha wilaya ya Shinyanga mjini Zenna Gulaam amesema wameona  vyema siku hiyo ya wanawake duniani kuiadhimisha katika kituo hicho cha watoto albino, ikiwa wao kama wazazi wana uchungu sana kusikia watoto hao wakiendelea kuuawa na kukatakatwa viungo vyao, hali iliyowafanya kuiomba serikali watu wanaotekelza mauji hayo wanyongwe-picha na Marco Maduhu-Malunde1 blog
Mwalimu Loyce Daudi ambaye pia mlezi wa watoto hao akiwashukuru akina mama hao kwa kufika katika kituo hicho na kuwapunguzia changamoto ya uhaba wa chakula na kuwaomba watu wengine wenye mapenzi mema kuwasaidia watoto hao-picha na Marco Maduhu-Malunde1 blog
Mwalimu Loyce Daudi akimshukuru mwenyezi mungu kwa kuendelea kusaidia watoto hao wanaoishi katika mazingira magumu waliotelekezwa na wazazi wao mara baada ya kukabidhiwa katika kituo hicho na kutorudi tena hali inayowafanya watoto hao waishi kwa kutegemea wasamaria wema-picha na Marco Maduhu-Malunde1 blog
 Watoto wakiwa katika kituo hicho leo-picha na Marco Maduhu-Malunde1 blog
Viongozi mbalimbali wa BAWACHA wakiwa kwenye kituo cha  Buhangija-picha na Marco Maduhu-Malunde1 blog

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
أحدث أقدم