MWALIMU ALIYEHIFADHI MALUNDO YA KINYESI CHUMBANI KWAKE ABAINIKA KUWA NA MATATIZO YA AKILI

Mwalimu wa shule ya Sekondari Kibasila, Gaudensia Albert aliyekuwa akihifadhi kinyesi ndani kwake kwa miaka miwili amepelekwa Hospitali ya Muhimbili baada ya daktari wa Hospitali ya Temeke kubaini ana matatizo ya akili.

Mwalimu Mkuu Msaidizi wa Shule hiyo, Kyando amesema baada ya kugundulika kwa tukio hilo walimpeleka Hospitali ya Temeke kwa kuangalia afya yake ambapo daktari akasema ana tatizo la akili, wakamuhamishia Muhimbili.
Baada ya kufikishwa Muhimbili madaktari walimpatia dawa ambazo anatumia mpaka sasa pamoja na ushauri.

“Sisi bado tunamhitaji kutokana na tatizo la uhaba wa walimu wa sayansi ulioko nchini”—alisema Mwalimu Kyando na kuongeza kuwa mbali na tatizo la kukutwa na kinyesi bado mwalimu huyo alikuwa anafundisha vizuri.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post