WILAYA YA NYANG'HWALE MKOA WA GEITA YATOA MSAADA KWA WAHANGA WA MVUA YA TONADO KAHAMA


Misaada mbalimbali kwa wahanga wa mvua  ya Tonado iliyoambataba na  upepo na mawe yanayodaiwa kuwa na uzito wa kil0 20 imeendelea kutolewa kwa wahanga ambapo leo mkuu wa wilaya ya  Nyang’wale mkoani Geita Ibrahim Marwa akiwa ameambatana na viongozi wa halmashauri hiyo amekabidhi msaada wa vyakula mbalimbali ikiwemo magunia 37 ya mahindi,unga wa sembe kilo 180,mchele kilo 70,mafuta ya kula lita 74,chumvi kilo 110,dagaa debe moja-picha zote na Kadama Malunde-Malunde1 blog

 
Kushoto ni  mkuu wa wilaya ya Geita ya  Nyang’wale mkoani Geita Ibrahim Marwa akizungumza wakati wa kukabidhi msaada wa chakula na vitu vingine kama vile madaftari,sabuni,mapanga na furushi la nguo na viatu.
 
 Halmashauri ya Nyang'wale ni ya kwanza kupeleka msaada kwa wahanga hao kati ya halmashauri zote nchini Tanzania
 
  Mkuu wa wilaya ya  Nyang’wale mkoani Geita Ibrahim Marwa( aliyevaa miwani) akikabidhi mfuko wa unga kwa mkuu wa wilaya ya Kahama Benson Mpesya anayepokea misaada mbalimbali kutoka watu mbalimbali kwa niaba ya serikalli na wahanga wa mvua ya upepo na Mwakata Kahama iliyonyesha  mapema mwezi huu
Kushoto ni mkuu wa wilaya ya Kahama Benson Mpesya akiwashukuru viongozi mbalimbali wa halmashauri ya
wilaya ya  Nyang’wale mkoani Geita waliokuwa wameambatana na mkuu wa wilaya hiyo Ibrahim Marwa.Mpesya alisema halmashauri hiyo kutoka nje ya mkoa wa Shinyanga imekuwa mfano mzuri kwa kuona umuhimu wa kusaidia wahanga wa mvua ya Tonado

Mkuu wa wilaya ya  Nyang’wale mkoani Geita akipeana mkono na mkuu wa wilaya ya Kahama Benson Mpesya

Mkuu wa wilaya ya  Nyang’wale mkoani Geita akipeana mkono na mkuu wa wilaya ya Kahama Benson Mpesya baada ya kumaliza zoezi la kukabidhiana misaada hiyo

Viongozi kutoka halmashauri ya wilaya ya
Nyang’wale mkoani Geita wakiwa katika picha ya pamoja na mkuu wa wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga-picha zote na Kadama Malunde-Malunde1 blog

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
أحدث أقدم