Makubwa!! COMPUTER ILIMSUMBUA SANA JAMAA,AKAPANDWA HASIRA AKAIPIGA RISASI MARA NNE

 
Mwanamme mmoja kwenye mji wa Colorado nchini Marekani huenda akachukuliwa hatua za kisheria kufuatia kisa ambapo alikasirishwa na kompyuta yake kisha akaitoa nje na kuifyatulia risasi mara nane.


Polisi wanasema kuwa Lucas Hinch alikuwa na matatizo ya kiteknolojia ndipo akaipeleka kompyuta hiyo upande wa nyuma ya nyumba yake na kuiharibu ambapo alikamatwa muda mfupi baadaye.

Vyombo vya habari vilisema kuwa alichoka na kusumbuliwa na kompyuta yake lakini hakufahamu kuwa alikuwa akivunja sheria alipoiadhibu kwa risasi.

Gazeti moja lilisema kuwa wakati herufi za ctrl+alt+delete zilifeli , bwana Hinch alishikwa na hasira nna kuamua kulipiza kisasi kwa kuiharibu Kompyuta hiyo hadi kiwango ambacho haiwezi kutumika tena

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com