BAADA YA RAIS MAGUFULI KUFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA MUHIMBILI..HII NI HABARI NJEMA

Siku ya tatu baada ya Rais Dk Magufuli kuingia Ikulu na kuanza kazi alifanya ziara za kushtukiza katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili ikiwa ni baada ya kumaliza ziara katika Wizara ya Fedha siku moja baada ya kuapishwa.

Baada ya kutembelea hospitali ya Muhimbili alifanya mabadiliko ikiwa kumsimamisha kazi Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali hiyo Hussein Kidantu sambamba na kutaka mashine za CT Scan na MRI zifanyiwe ukarabati baada ya kukaa miezi miwili bila kuhudumia wagonjwa kutokana na ubovu wake.

Kamati mpya tendaji ya hospitali hiyo ilikutana jana na mara moja kuitisha wataalam ambao leo walianza kazi ya utengenezaji wa mashine hizo.

Taarifa mpya kutoka kwa Mkuu wa kitengo cha mawasiliano ya umma Aminiel Eligaisha amesema ni kweli mashine za MRI tayari zimeanza kufanya kazi na mashine za CT Scan bado zipo katika matengenezo na zitaanza kufanya kazi wakati wowote kuanzia sasa.

Barua ilisomeka hivi…

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post