KAULI YA MCHEKESHAJI MASANJA MKANDAMIZAJI BAADA YA KUUKOSA UBUNGE JIMBO LA LUDEWA KWA DEO FILIKUNJOMBE

List ya mastaa wa Bongo Tanzania ambao walijitosa na kujipanga kwenye foleni ya kuusaka Ubunge iliongezeka baada ya mchekeshaji kutoka Kundi la Orijino Komedi, Masanja Mkandamizaji nae kujitosa kwenye foleni hiyo.


Masanja alithibitisha kwamba kazi ya Ubunge anaiweza >>> “Orijino Komedi ipo, mimi sio member wa kundi, mimi ni mwanzilishi.. siwezi kuacha Komedi, mbona nilikuwa Mchungaji na sikuacha Komedi.. nitakuwa Mbunge, Komedi na Church…” >> Hii ni siku chache zilizopita kwenye exclusive interview na millardayo.com pamoja na #Amplifaya.


Masanja akiwa kwenye Ofisi za Chama wakati wa mchakato wa Kura za maoni, Ludewa Njombe.

Kura hazikutosha kwake, maana yake ni kwamba kwenye Kura za maoni upande wa makada wa CCM Ludewa, Masanja hajafanikiwa kupita… lakini aliahidi pia hata kama akishindwa bado ataendela kumpa support yule atakaepita.

Kwenye ukurasa wake wa Twitter, Masanja ameandika haya kukubali matokeo >>>> “Ludewa ….. Dah! Najipanga nitarudi tena. Sasa ni muda wa kumpigia kampeni aliyepita ili akatuwakilishe Bungeni. #HapaKaziTu” >>> @mkandamizaji


Marehemu Deo Filikunjombe (katikati) ndio aliyekuwa Mgombea Ubunge wa Jimbo la Ludewa, baada ya kufariki kwa ajali ilibidi Uchaguzi wa Mbunge usogezwe mbele.

Jimbo la Ludewa liko kwenye list ya Majimbo ambayo Uchaguzi wa Wabunge haukufanyika kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kufariki kwa Wagombea Ubunge.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post