Picha!!! TAARIFA RASMI KUHUSU AJALI BASI LA NEW FORCE KUUA WATU 12 PAPO HAPO BAADA YA KUGONGANA NA LORI LA MBAO



Watu 12 wamefariki dunia papo hapo baada ya lori la mbao lililokuwa likitokea Njombe kwenda jijini Dar es Salaam kupasuka tairi na kugongana na basi la abiria la New Force lililokuwa linatokea jijini Dar es Salaam kuelekea Tunduma leo katika eneo la Kitonga wilaya ya Kilolo mkoani Iringa.


Kwa mujibu wa kamanda wa polisi mkoa wa Iringa, kamishina msaidizi wa polisi Ramadhani Mungi amesema  waliofariki ni wanaume nane na wanawake wanne majeruhi ni 28 ambao wengine wamepelekwa Iringa mjini na wengine wako katika hospitali ya wilaya Kilolo-Iringa.


Aidha Kamanda Mungi amewataka madereva kuwa makini hasa katika kipindi hiki cha sikukuu na kuepuka mwendo kasi pamoja na kutoa taarifa pale vitendo kama hivyo vinapotokea













Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post