Askari wa Usalama Barabarani, Ally Kinyogoli Auawa kwa Kupigwa Risasi Huko Pwani

 
Watu wasiojulikana wakiwa na pikipiki aina ya Boxer,usiku wa kuamkia leo wamemuua kwa kumpiga risasi kadhaa katika sehemu mbalimbali za mwili wake askari wa Jeshi la Polisi kitengo cha usalama barabarani, Ally Kinyogoli nyumbani kwake Mwandege, Mkuranga mkoani Pwani.


Baada ya kumuua, watu hao walitokomea kusikojulikana bila kuchukua kitu chochote.

Kinyogoli alijizolea umaarufu katika kipindi cha redio One kila siku asubuhi alipokuwa akitoa taarifa za hali za barabarani zikiwemo njia zenye foleni kwa wakazi wa jijini.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
أحدث أقدم