Angalia Picha- Rais Magufuli Amuapisha Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 04 Juni, 2016 amemuapisha Mhe. Gerson John Mdemu kuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali.


Kabla ya kuteuliwa kuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mhe. Gerson John Mdemu alikuwa Karani wa Baraza la Mawaziri (Cabinet Clerk)

Mhe. Gerson John Mdemu amechukua nafasi iliyoachwa wazi na Mhe. Dkt. Tulia Ackson ambaye ni Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam
04 Juni, 2016


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post