Mfanyabiashara Afikishwa Mahakamani Kwa Tuhuma za Kumuua Mkewe na Kusingizia Kajiua Mwenyewe

Mfanyabiashara mwenye asili ya Uingereza Richard Alden amefikishwa Mahakamani akituhumiwa kuhusika na mauaji ya Grace Wangechi Kinyanjui ambaye alikuwa ni mke wake wa pili katika nyumba yake ya kifahari nchini Kenya amefikishwa mahakamani baada ya polisi kukataa madai yake kuwa alijiua mwenyewe.

Mfanyabiashara huyo baada ya tukio alimpeleka Grace Wangechi Kinyanjui hospitalini akidai kajipiga risasi mwenyewe na Kinyanjui alifariki muda mfupi baadae kutokana na majeraha makubwa aliyoyapata. Mtuhumiwa amefikishwa mahakamani na ataendelea kushikiliwa siku tano zaidi wakati polisi wakiendelea na uchunguzi.

Kamanda wa polisi Japheth Koome amesema wanandoa hao wamekuwa kwenye mahusiano na walikuwa wanaishi pamoja pia majeraha ya Kinyanjui yanaendana na mauaji na kulikuwa na jeraha la risasi nyuma ya kichwa chake pia alikuwa na majeraha matatu upande wa kushoto wa shingo yake.





Grace Wangechi Kinyanjui wakati wa uhai wake

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post