Sheria ya Mtandao Yanasa Mwingine..Huyu Kamtukana Rais Magufuli kwenye WhatsApp

Sheria ya Makosa ya Kimtandao inaendelea kushika kasi, mwingine tena aingia matatani baada ya kubainika kutumia Lugha mbaya dhidi ya Rais kwenye mtandao wa WhatsApp.


Leonard Mulokozi Kyaruzi anakabiliwa na kesi baada ya kuandika maneno ya kumtukana Rais John Pombe Magufuli si kwenye Facebook kama Isaac Abubakar wa Arusha, bali ni kwenye WhatsApp – Yes ulidhani kwenye magroup unaweza kutukana unavyotaka?


Kwa mujibu wa hati ya mashtaka iliyotolewa Jumanne hii, Kyaruzi anadaiwa kutoa kauli hiyo ya kejeli kwenye WhatsApp June 2. 
Aliandika: Hivi huyu Pombe ni kwamba hana washauri? Hashauriki? Au ni zuzu? Bwege sana huyu jamaa, he doesn’t consider the law in place before opening his mouth!. Au na yeye anaumwa ugonjwa wa Mnyika?”
 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post