Watu Watatu Wamepoteza Maisha Baada ya Kula Mihogo Yenye Sumu Huko Morogoro


Katika hali ya kusikitisha watu watatu wakazi wa kijiji cha Kauzeni wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro wamekufa baada ya kula mihogo inayosadikiwa kuwa na sumu huku wengine wawili wakilazwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Morogoro na mmoja kupata nafuu na kuruhusiwa.


Akizungumza na ITV akiwa hospitalini hapo mara baada ya kunusurika kifo Joshua Msiani amesema anachokumbuka walikuwa katika shughuli zao za kufyatua tofali ndipo wenzake wakamkaribisha mihogo ya kuchemsha na baada ya kula ndipo ghafula hali ikawa mbaya na kujikuta yupo hospitalini.



Kwa upande wa Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro Ulrich Matei amethibitisha kutokea kwa vifo hivyo ambapo amesema mamlaka husika zimechukua sampuli ya mihogo na uchunguzi unaendelea ili kubaini chanzo cha vifo hivyo .




Waliofariki dunia kwa tukio hilo ni Daudi Hermani mkazi wa Kauzeni, Omary Mohamed pamoja na Hamisi Mohamed ambao ni mapacha.
Chanzo-ITV

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post