FILAMU YA MWISHO KUCHEZA MAREHEMU MASOGANGE KUTOKA DESEMBA 15, 2018

Msanii wa Filamu Bongo, Rammy Galis anatarajia kuzindua filamu yake mpya inayokwenda kwa jina la Hukumu.

Katika filamu hiyo Rammy Galis amecheza na aliyekuwa Girlfriend wake Marehemu Agnes Gerald maarufu kama Masogange.

Sio Masogange pekee yake bali waigizaji wengine wakubwa na wakali wameshiriki kwenye filamu hiyo itakayozinduliwa kwa mara ya kwanza December 15, 2018 City Mall, Dar es Salaam.

Agness alipata umaarufu mkubwa pindi alipotokea katika video ya msanii Belle 9 ambayo ilikwenda kwa jina la Masongange ndipo na yeye kuanza kutumia jina hilo. Masogange alifariki April 20, 2018 katika hospitali ya Mama Ngoma iliyopo Mwenge, Dar es Salaam.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post