HALMASHAURI YA GEITA MJINI YATOA MKOPO WA BILIONI 1.6 KWA VIJANA, WANAWAKE NA WALEMAVU


Mbunge wa Geita mjini ambaye pia ni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu amesema Halmashauri ya mji wa Geita hadi kufikia mwezi Julai mwaka huu tayari  imeshatoa mkopo wa Shilingi bilioni 1.6 kwa ajili ya wakinamama, vijana na walemavu  kwa lengo la kutimiza  adhima ya Serikali ya awamu ya tano chini ya uongozi wa  Rais John Pombe Magufuli.

Amesema lengo la kutoa mkopo huo  ni  kutatua changamoto ya ukosefu wa ajira na kuweza kuinua kipato cha wananchi kwa kunufaika na miradi mbalimbali na hatimae kuweza kujikwamua kiuchumi.

Hayo ameyasema kwenye mkutano wakati akizungumza na wananchi wake kuhusu ahadi mbalimbali alizozitekeleza ikiwemo ya kutoa mkopo wa shilingi bilioni 1.6   kwa vikundi mbalimbali  kwa lengo la kupunguza umasikini katika jamii katika mkutano huo  uliofanyika katika kata ya Ihanamiro wilaya ya Geita mkoani Geita.

Mhe.Kanyasu amewaeleza wananchi hao kuwa kutokana na uhusiano mzuri uliopo miongoni mwa madiwani katika Halmashauri hiyo wameweza kutoa mkopo huo. Hata hivyo amesema kuwa mikopo hiyo itasaidia katika uanzishwaji wa viwanda vidogo vidogo ambavyo vitasaidia kutengeneza ajira na kukuza uchumi

Akizungumza katika mkutano huo,Mhe.Kanyasu amesema anajisika fahali ya  kutoa mikopo hiyo kwa vikundi ikiwa ni moja ahadi alizozitimiza za kuhakikisha mwananchi wake wanajihusisha kwenye shughuli za kiuchumi ili kupunguza umasikini kuanzia ngazi ya familia hadi taifa

Amesema kuwa kutokana na changamoto zilizoko  katika taasisi za fedha, ambazo hutoa mikopo kwa riba kubwa na kuhitaji dhamana ya nyumba na ardhi jambo ambalo linawakwamisha wakopaji hivyo serikali imeamua kutoa mikopo ya masharti nafuu.

Aidha amesema mikopo  hiyo itawasaidia makundi hayo kuweza  kuongeza mitaji na kutoa ajira ndani ya jamii.

Aidha, Mhe, Kanyasu amesema katika awamu ya pili ya utoaji mkopo  wataongeza viwango vya mikopo kwenye vikundi ambapo kila kikundi kitakuwa na uwezo wa kukopeshwa hadi kufikia shilingi milioni 20 tofauti na ilivyokuwa awali

Kwa upande wake, Diwani wa kata ya Ihanamiro,  Mhe. Joseph Lugaira amemueleza Mbunge huyo kuwa katika kata hiyo jumla ya vikundi 19 vimenufaika na mkopo huo kwa kuanzisha shughuli za kiuchumi.

Amesema vikundi hivyo vimekuwa vikifanya shughuli mbalimbali za kiuchumi ikiwemo biashara pamoja na kilimo ambapo anaamini wataweza kupata faida pamoja na kurejesha mkopo huo na kukopa tena.

Naye Diwani wa viti maalum, Mhe. Suzana Mashala  amewahimiza wanawake wasiogope kukopa kwani hawawezi kujiendeleza kiuchumi pasipo kukopa.

Vile vile, Diwani huyo alitumia fursa hiyo kuwahimiza wanawake waliokopa wajitahidi kurejesha mikopo hiyo mapema ili mikopo hiyo iweze kuwasaidia watu wengine lengo likiwa ni kuondokana na umasikini.

Kwa upande wake, Emalio Nyangabo ambaye ni kiongozi wa Kikundi cha Tuinuane, amesema   walipokea mkopo ambao umewasaidia kuinuka  kiuchumi, na kuwawezesha kufanya shughuli za uzalishaji mali na kuachana na kujihususha na vitendo visivyofaa katika jamii

Naye, Godson Maduka ambaye ni miongoni mwa vijana walionufaika wa mkopo huo amesema mkopo huo umewasaidia vijana wengi kujiepusha kujiingiza kwenye utumiaji wa madawa ya kulevya na unywaji wa pombe kupita kiasi.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
أحدث أقدم