
Chuo Kikuu cha Johns Hopkins nchini Marekani kimetangaza kuwa karibu watu 4,591 wamefariki dunia katika kipindi cha masaa 24 yaliyopita kutokana na virusi vya Corona na hivyo kufanya idadi ya waliokufa kwa ugonjwa huo nchini Marekani kufika 34,641.
Aidha taarifa mpya iliyotolewa na Chuo Kikuu cha Johns Hopkins imesema kuwa katika kipindi cha masaa 24 yaliyopita karibu watu elfu 30 wengine wameambukizwa virusi vya Corona nchini humo.
Social Plugin