WAZIRI NCHEMBA AWAPONDA BAADHI YA WABUNGE WA UPINZANI KUSUSIA VIKAO VYA BUNGE


Waziri wa Katiba na sheria Mhe.Mwigulu Nchemba amesema kitendo cha baadhi ya Wabunge wa Upinzani kususia vikao vya Bunge  kwa kuogopa Corona ni ishara ya kutengeneza madaraja na mpango wa kushusha uchumi wa nchi.

Waziri Nchemba amesema hayo jana Bungeni jijini Dodoma wakati akichangia hotuba ya     wizara ya       Viwanda na Biashara ya makadirio na matumizi kwa mwaka wa fedha,2020/2021 ambapo amewataka Watanzania kuacha kusikiliza miluzi  ambayo inapotosha taifa.

Waziri Nchemba amesema  Maisha ya Watanzania mara nyingi hayana akiba hivyo kitendo cha watanzania kujifungia ndani  bila kufanya kazi kwa tahadhari ya Corona  kama wanavyoshauri baadhi ya wabunge wa Upinzani panaweza kutengeneza majanga mengine hivyo wanatakiwa  kufuata ushauri uliotolewa na Rais Dkt.John Pombe Magufuli wa kuchapa kazi na kuondoa hofu juu ya Corona na kubainisha kuwa janga halikimbiwi.

Waziri Nchemba ameteuliwa na Rais Dokt John Pombe Magufuli hivi karibuni kuiongoza Wizara ya Katiba na Sheria tukio lililofanyika Mjini Chato mkoani Geita baada ya aliyekuwa waziri wa Wizara hiyo  Dkt.Balozi Augustine Mahiga  kufariki Dunia


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post