
Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za mitaa (TAMISEMI) ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Ukonga, Mwita Mwikwabe Waitara leo amechukua fomu ya kuomba kugombea Ubunge jimbo la Tarime vijijini.

Nyerere Jackson Mwera akichukua fomu kugombea Ubunge Jimbo la Tarime mjini
Na Dinna Maningo - Malunde 1 blog TarÂime.
Wanachama 42 wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wamejitokeza kuchukua fomu za kuomba kugombea Ubunge Jimbo la Tarime mjini na Tarime vijijini kupitia CCM huku idadi ya wanawake ikiwa ndogo ikilinganishwa na wanaume.
Akizungumza na Malunde 1 blog Katibu wa chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Tarime mkoani Mara,Hamis Mkaruka amesema kuwa hadi kufikia siku ya leo Julai 15, 2020 wanawake waliochukua fomu ni watano pekee ,wanaÂume wakiwa 37.
Mkaruka alisema kuwa kwa upande wa Jimbo la Tarime mjini wanawake ni Suzy Chambili,Monica AnicÂet na Dr.Veronica Robert ambapo Jimbo la Tarime vijijini ni Joyce Ryoba na Dr. Stella Faustine
Naye Naibu Waziri OfÂisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za mitaa (TAMISEMI) aÂmbaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Ukonga,MÂwita Mwikwabe Waitara amechukua fomu ya kuomba kugombea UbÂunge jimbo la Tarime vijijini.
Makada wa CCM waliochukua fomu kuomba kugombea Ubunge hadi kufikia siku ya leo majira ya saa nane mchana waliochukÂua fomu jimbo la TarÂime vijijini ni 24 na Tarime mjini wakiwa 18 .
Wengine waliochukua fomu kwa jimbo la Tarime mjini ni Hezbon Mwera, Jackson RyoÂba, Dr.Edward MachagÂe,Julius Mtatiro EngÂ.William Machage,CheÂche Andrew,Julius LaÂbaran,Samwel Marwa,EÂvangel Otieno,Michael Kembaki,Jeremia Seba,Gerald Martine,MÂwita Joseph,Zakayo Wangwe na Manchare HeÂche Siguta.
Kwa jimbo la Tarime vijijini ni Joseph Nyahende,Yusuph WambuÂra,Chacha Masero,John Gimunta,Mwita Jacob Marwa,Wambura SagiÂre,Thomas Chacha MwiÂta, Musa Raphael, NyÂerere Mwera,Nyamhanga David,Dr.Abdalah Chigo,Dr.Paul MwikwabÂe,Mordikae Moset,EliÂakimu Maswi,Nicodemas Keraryo,James BwirÂe,Peter Amos Bhusene Frank Mniko,Lucas Magoti,Samwel Mantarya na Ngocho Darius.
Katibu wa CCM wilaya ya Tarime Hamis MkaÂruka alisema kuwa waÂnawake wanapaswa kuoÂndoa hofu na badala yake wajitokeze kugoÂmbea nafasi za Ubunge na Udiwani.
Social Plugin