BASI LA HAPPY NATION LAPATA AJALI MOROGORO, WANNE WAJERUHIWA


Lori la basi yaliyogongana Morogoro

Watu wanne wamejeruhiwa katika ajali ya barabarani iliyotokea eneo la Mkambalani wilayani Morogoro, ikihusisha basi la Happy Nation lenye namba za usajili T 702 DGF likilokuwa linatokea Dar es Salaam kuelekea Bukoba na lori la mizigo lililokuwa linatoka Zambia kwenda Dar es Salaam.


Ajali hiyo imetokea leo Julai 20, 2022, majira ya saa 3:00 asuhubi, ambapo baadhi ya abiria waliokuwa kwenye basi hilo wamesema kuwa kilichosababisha ni kutozingatiwa kwa sheria za barabarani wakiomba jeshi la polisi kitengo cha usalama barabarani kuongeza umakini ili kupunguza ajali zisizo za lazima.

Mkuu wa Upelelezi mkoa wa Morogoro ACP Ralph Meela, amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo ambapo chanzo cha ajali kinadaiwa kuwa ni uzembe wa dereva wa basi hilo Hassan Abdallah ambaye alikuwa akijaribu kulipita gari lingine bila kuchukua tahadjari na kusababisha ajali hiyo.

Chanzo - EATV

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post