RC MWASSA ARIDHISHWA UJENZI JENGO LA DHARURA HOSPITALI YA WILAYA KARAGWE

Na Mariam Kagenda - Kagera
Ikiwa ni mwendelezo wa ukaguzi wa miradi ya maendeleo Wilaya ya Karagwe mkoa wa Kagera Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. Fatma Mwassa amepongeza ukamilishaji majengo ya kutolea huduma katika hospitali ya Wilaya ya Karagwe na utendaji kazi.

Akizungumza baada ya kukagua jengo hilo la huduma ya dharula Mhe. Mwassa ametoa wito kwa watumishi wa sekta ya afya kufanya kazi kwa kukidhi matakwa ya wananchi ikiwemo kuwapa huduma bora na kuwaelewesha juu ya umuhimu wa kupata huduma za matibabu kwa wakati.


Amesema kuwa anawapongeza kwa usimamizi mzuri pamoja na usafi wa Mazingira ya Hospital nzima ikiwemo utunzaji wa miundombinu ambapo hospitali nyingi ukitembelea unakuta Mazingira hayaridhishi.


Serikali kupitia TAMISEMI imetoa fedha shilingi bilioni 3.5 kuhakikisha wanakuwa na hospitali ya kisasa ambayo haiwatofautishi na hospitali nyingine zilizoko Mwanza, Dar es salaam na Dodoma kinachotakiwa ni kufanya kazi kwa kukidhi matakwa ya wananchi.

Aidha, amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa hospitali hiyo ambayo imewaondolea kero wananchi kutembea umbali mrefu kufuata huduma ya afya.

Kwa upande wao baadhi ya wananchi wamesema wanaridhishwa na huduma zinazotolewa katika Hospitali hiyo na hakuna wasiwasi, ukilinganisha na miaka ya nyuma ambapo walilazimika kufuata huduma nyingi katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando iliyopo Mwanza.

Wamesema kuwa kipindi cha nyuma changamoto kubwa ilikuwa ni kupata huduma nzuri za afya ambapo kwasasa Serikali imerahisisha huduma zote za upasuaji, masuala ya upumuaji hakuna tofauti tena kati ya Bugando na Karagwe, kwa ujumla wananchi naridhishwa na huduma zote zinazotolewa, changamoto ndogondogo za uwepo wa watumishi wanaamini Serikali itazitatua.

Katibu wa Hospitali, Samson Hingi ameeleza kuwa ujenzi wa Hospitali hiyo ulianza mwaka 2019 na kwasasa huduma nyingi zinapatikana hospitalini hapo hivyo gharama za wananchi kupewa Rufaa na kufuata huduma za afya mbali zimepungua. Mpaka sasa asilimia 60 ya vifaa tiba vya kisasa vimefungwa na wagonjwa wanapata huduma nzuri.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post