MWENGE WA UHURU WATUA KAGERA, KUPITIA MIRADI 57 YA BILIONI 26

Na Mariam Kagenda - Kagera
Mkoa wa Kagera tayari  umepokea Mwenge wa uhuru leo Agosti 8,2023  kutoka mkoa wa Geita ambao wamehitimisha   mbio za Mwenge na kuukabidhi mkoa wa Kagera.

Makabidhiano ya Mwenge  wa uhuru kati ya mkoa wa Kagera na Geita yamefanyika  katika kata ya Nyakabango wilayani   Muleba mkoani Kagera  ambapo mwenge huo utaanza kukimbizwa katika wilaya ya Muleba .

Wakati akipokea Mwenge huo mkuu wa mkoa wa Kagera Mh Fatma Mwassa amesema kuwa  hali ya usalama katika mkoa huo ni salama  na mwenge wa uhuru utakimbizwa katika halmashauri zote nane za mkoa huo kwa umbali wa Kilomita 1200.4.


Amesema kuwa mkoa wa Kagera utawapa ushirikiano wa kutosha wakimbiza mwenge kitaifa  mpaka pale mkoa huo utakapohitimisha mbio za mwenge na  kuukabidhi mwenge  huo mkoa wa  Geita Agosti  16 ,2023 ambapo ukiwa mkoani Kagera utazindua,kukagua,kutembelea jumla ya miradi 57 yenye thamani ya  shilingi Bilioni 26.

Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Geita Martine Shigera wakati akikabidhi mwenge huo kwa mkuu wa mkoa wa Kagera Fatma Mwassa  amesema kuwa   mwenge wa uhuru ulipokuwa katika mkoa huo  uliweka mawe ya msingi,kufungua,kuzindua na kukagua jumla ya miradi 59 yenye thamani ya zaidi ya shilingi  bilioni 29.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post