Tanzia : MWENYEKITI WA ZAMANI WA SIMBA SC AYOUB CHAMSHAMA AFARIKI DUNIA

 

Ndugu Soud Ayubu Chamshama
wa Chang'ombe Dar es salaam 
Anasikitika kutangaza kifo cha Baba 
Yake mzazi,  Mzee Ayubu Salehe Chamshama, 
Kilichotokea tarehe 11 Agosti 2023
nchini India alikokuwa kwa matibabu.

Mazishi yanatarajiwa kufanyika siku ya Jumanne tarehe 15 Agosti 2023 kijijini kwao Kilole, Lushoto, Mkoani TANGA.

Msiba upo nyumbani kwa marehemu Chang'ombe Maduka Mawili Dar es salaam.

Habari ziwafikie Ndugu, Jamaa na marafiki popote pale walipo.

Enzi za uhai wake Marehemu Chamshama alishika nyadhifa mbalimbali. Alikuwa Meneja Mkuu wa kampuni ya Tanzania Tea Blenders, vilevile alihudumu kwa muda mrefu kama Mwenyekiti wa klabu ya Simba SC na pia alikuwa Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Temeke.

Inna Lillahi wa inna ilayhi raji'un

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post