MFUMO WA REEFER CONTAINERS KUNUFAISHA WAKULIMA



Kukamilika kwa Mfumo wa Makasha yanayotumia Umeme kwa ajili ya kuhifadhi bidhaa ambazo zinaweza kuharibika kutokana na Joto kutawezesha wakulima mbalimbali wanaotaka kusafirisha bidhaa hizo kwenda nje ya nchi kupitia Bandari ya Tanga Kusafirisha bidhaa hizo bila kuharibika.

Hayo yamesemwa na Afisa Masoko na Huduma kwa Wateja wa bandari ya Tanga Habiba Godigodi wakati wa Maonyesho ya Wakulima Nanenane kanda ya Mashariki Mjini Morogoro ambapo Bandari ya Tanga wanashiriki ili kuweza kutangaza fursa zilizopo.

Habiba alisema kuwa kulikuwa na changamoto kwa Wakulima wanaosafirisha bidhaa kama Matunda mbalimbali pamoja na Maua kushindwa kusafirisha bidhaa hizo kutokana na kutokuwepo kwa njia sahihi ya kuhifadhi bidhaa hizo hivyo bandari ya Tanga imetengeneza  eneo maalum la  kuhifadhia makasha yenye mfumo wa umeme ili waweze kuhifadhi wakati wanapotaka kusafirisha bidhaa hizo.

"Hivyo ni fursa kwenu wafanyabiashara kuitumia Bandari ya Tanga kusafirisha bidhaa hususani wakulima wa matunda mbalimbali pamoja na maua kutokana na uwepo wa sehemu sahihi ya kuhifadhi bidhaa hizo  kupitia makasha yenye mfumo wa umeme "Alisema 


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post