STAMICO YAWA MKOMBOZI KWA WAZALISHAJI WA CHUMVI NCHINI

#Shamba darasa kuwafundisha wazalishaji wa chumvi Lindi na Mtwara

Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) limeanza kushughulikia changamoto za wazalishaji wa chumvi nchini kwa ajili ya kuongeza uzalishaji wa chumvi nchini kuwa wa tija na manufaa.

Hayo amesema Meneja Uwezeshaji uchimbaji mdogo Tuna Bandoma wakati wa Maonesho ya Madini na Fursa za Uwekezaji akizungumza katika Kongamano la Wadau wa Chumvi lililofanyika Agosti 21, mkoani Lindi.

“Mikakati iliyopo ni mahususi kwa ajili ya kuja na suluhisho ili kutatua changamoto zilizopo ambayo tumehusisha wadau, tunakua na uelewa wa pamoja katika kushughulikia changamoto za wazalishaji wa chumvi nchini, “ amesema Bando.

Aidha, amesema STAMICO inaendelea na hatua mbalimbali ikiwemo hatua za haraka za kiwanda cha kusafisha chumvi katika wilaya ya Kilwa na tayari Mkoa umeonesha eneo kwa ajili ya utekelezaji wa kujenga kituo hicho.

Ameongeza kuwa, katika shamba darasa la STAMICO wazalishaji wa chumvi watafundishwa namna mbalimbali ya kuyafikia masoko kupitia ubora ili kuzalisha chumvi iliyo bora kufikia masoko ndani na nje ili kuvutia wawekezaji

Mafunzo hayo ni moja ya utekelezaji wa kalenda ya mafunzo kwa wachimbaji wadogo inayofanywa na STAMICO.

Awali Kongamano hilo na mafunzo ya wazalishaji chumvi lilifunguliwa na Mhe. Naibu Waziri wa Madini Dkt.Stephen Kiruswa Kwenye Viwanja vya kilimahewa Wilaya Ruangwa Mkoani Lindi.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post