CCM TANGA YAKAZIA VIONGOZI NA WATENDAJI WOTE WAACHE KUTUMIA MABAVU KWA WANANCHI

Na Hadija Bagasha Tanga.

MWENYEKITI  wa Chama Cha  Mapinduzi 'CCM' Mkoa wa Tanga Rajab  Abdulrahman  ameendelea kusisitiza viongozi kutekeleza agizo la Rais Dkt Samia Suluhu Hassan alilolitoa hivi karibuni kwa wakuu wa wilaya na mikoa   kuwataka viongozi na watendaji wote kuacha kutumia mabavu kwa wananchi wanaowaongoza.

Kauli hiyo ameitoa  wilayani Handeni katika ziara yake alipofika kukagua ujenzi wa Zahanati ya kijiji cha  Kibaya kata ya Misima ambapo  licha ya kutoa Milion 4  tangu February 2024 kwaajili ya ununuzi wa Tofali umeshindwa kuanza kwa  wakati kutokana na mvutano baina ya wananchi huku wakidai kutokushirikishwa  kwenye miradi pamoja na kutishiwa kupelekwa Polisi  na viongozi wao pale wanapohoji kinachoendelea.

Rajabu aliwataka viongozi hao  wakae  pamoja na wananchi wa kijiji hicho cha Kibaya ili kuondoa  tofauti zilizopo ambapo kati ya vitongoji vinne vilivyopo ni wananchi wa vitongoji viwili pekee ndio wanaoshiriki katika ujenzi wa zahanati hiyo.

" Viongozi wenye kutumia ubabe Mheshimiwa Rais hataki kuwaona kabisa  viongozi hao  , ubabe wa nini ? wewe unawaongoza watu wenye akili zao timamu na maarifa  kama wanakosea wajibu wako kama kiongozi  unapoona wananchi wanalalamika ujue kuna tatizo sio bure " alisema Rajabu.

"Kijiji hiki kina vitongoji vinne zahanati hii ni ya vitongoji vyote  haiwezekani wananchi wa vitongoji fulani hawashiriki wanashughulika wengine  lazima wananchi wa vitongoji vyote nao washiriki  katika mradi huu kutoa nguvu zao,viongozi niwaelekeze twendeni tukakae nao kwanini hawashiriki kisha baada ya hapo tuondoe tofauti hizo,kuhakikisha kwamba mgogoro huu unamalizika lakini mradi huu lazima  uendelee  kama tulivyokusudiwa ili kuwapunguzia na kuwaondolea wananchi  adha hizi za kukosa huduma ya afya karibu"

"Nina timu yangu inayopita  mkoa mzima huu wa Tanga miradi yote ya serikali tunapita kuangalia mambo   yanaendaje  ni kweli wananchi hawa hawashirikishwi  katika mradi huu na katika miradi mingine , katika maelekezo ninayoyatoa kuanzia sasa lazima wananchi  hawa washirikishwe  hatua moja baada ya nyingine lazima wananchi wote  washiriki kutoa nguvu zao katika mradi huu"

Awali akizungumza mmoja wa wananchi wa kijiji hicho cha Kibaya Hamza Mazimu alisema kuwa  eneo hilo hakuna huduma za afya  karibu,hivyo inawabidi kutembea kilomita  saba,sawa na kilomita  14 kwenda na kurudi kata ya jirani kufuata huduma ya afya.

Alisema kumekuwa na changamoto ya kutokushirikishwa kwa wananchi wa Kijiji hicho katika utekelezaji wa miradi mbalimbali hali ambayo imekuwa ikichangia mvutano baina yaona viongozi  kocha ya kukosa huduma za afya kwa kipindi cha muda mrefu hatua ambayo imekuwa ikiwafanya kutembea umbali wa kilomota 7 kufuata huduma katika kata za jirani.

"Wananchi wa Kijiji Cha Kibaya   walichanga nauli zao kwenda mpaka ofisi ya Mkurugenzi kudai Zahanati kwa sababu wakina mama  wanateseka Sana, tunachifanywa Sasa hivi ni kuwajibishwa na sio kushirikishwa  hatuwezi kupelekea hivyo na ukizingumza  unaweza kupelekea Polisi kwaajili ya kudai haki za wanakijiji lakini kama tutashirikiahwa tutachangia mpaka kuhakikisha Zahanati inasimama" alisema Mazimu

"Hapa inatubidi kutembea kilo saba kwenda kata ya jirani kufuata huduma za afya,wanawake ndio wanateseka zaidi kwa kutembea umbali mrefu,hivyo ujenzi wa zahanati hii ni muhimu sana kwetu ila mtendaji wa kijiji amekuwa ni kikwazo kwetu kufanikisha ujenzi huu", aliongeza.

Zahanati hiyo yakijiji cha Kibaya inayojengwa kwa nguvu za wananchi  tayari Mwenyekiti chama Cha Mapinduzi alichangaia kiasi Cha Milion 5.500,000 kwaajili ya ununuzi wa Tofali , ujenzi wa msingi pamoja na ununuzi wa mchanga ambapo tayari ujenzi huo umeshaanza.

Mkuu wa wilaya ya Handeni Albert Msando amekiri kuwepo mgogoro huo wa mvutano baina ya wananchi wa Kijiji hicho  waliokuwa wakizozana juu ya ujenzi wa Zahanati tangu Februari mwaka huu ambapo tayari ofisi yake kwa kushiriki na chama waliutatua na  hatimaye kufikia makubaliano ya kuanza kwa ujenzi.

"Mgogoro huu tunaufahamu alikuja afisa tarafa  tukaongea nao likapatikana suluhisho  baada ya hapo uliotokea mvutano mwingine ambao ulipelekea ofisi kufungwa  ukimhusisha mtendaji na Mwenyekiti wa Kijiji tukifanya nao kikao na tukatoa maelekezo kwamba kazi ianze na walituahidi baada ya siku Saba  watakuwa wameanza kichimba msingi" alisema Msando.

Mwenyekiti wa Kijiji hicho  Mohammed Fumira  amemshukuru Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Tanga Rajabu Abdulrahaman  kwa kuwasaidia kiasi cha   shilingi Milion 5.500,000  kwaajili ya ununuzi wa tofali, mchanga pamoja ujenzi wa msingi  katika eneo hilo lenye ukubwa wa hekali 10 wakitarajia kujenga pia na nyumba za wahudumu.

Kwa niaba ya wananchi wa Kijiji cha Kibaya   tunashukuru Sana Mwenyekiti wetu wa achama Cha Mapinduzi kwa  kutusaidia kiasi cha fedha shilingi Milion 5.500,000 kwaajili ya ujenzi wa Zahanati yetu wakina mama walikuwa wanateseka kutembea umbali mrefu kufuata huduma za afya  tunaahidi kuikamilisha ujenzi huu kwa nguvu za wananchi" 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post