WATUHUMIWA MAUAJI YA ASIMWE WAFIKISHWA MAHAKAMANI



Na Mwandishi Wetu, Kagera

Watuhumiwa tisa wa mauaji ya mtoto Asimwe Novart aliyekuwa na ualbino ambaye aliibwa nyumbani kwao Kamachumu may 30 mwaka huu 2024 ambapo June 17 mwaka huu 2024 mwili wake ulikutwa kwenye kalavati akiwa ameuawa na kukatwa baadhi ya viungo vyake,leo wamefikishwa katika mahakama ya Hakimu Mkazi Bukoba wakiwa chini ya ulinzi mkali kwa ajili ya kusomewa mashtaka yao

Mkuu wa mashtaka Mkoa wa Kagera Waziri Mangumbo akisaidiana na wakili wa serikali Erick Mabagala wamewasomea mashtaka yao watuhumiwa hao tisa kuwa wanakabiliwa na shitaka la mauaji ya makusudi huku akisema kuwa uchunguzi wa shauri hilo no 17740 la mwaka 2024 tayari umekamilika

Shitaka hilo limesomwa mbele ya Hakimu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Bukoba Elipokea Yona Wilson ambaye amesema Mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo hivyo washtakiwa hawakutakiwa kujibu chochote na wamerudishwa rumande mpaka July 12,2024 ambapo kesi yao itatajwa tena

Watuhumiwa hao tisa ni Elpidius Alfred Rwegoshora miaka 49 ambaye ni padri,Novat Venant miaka 24 ambaye ni baba wa mtoto,Nurdin Ahmada,Ramadhan Selestine,Rwenyagira Alphonce,Dastan Buchard, Faswiu Athuman,Gozibert Arikad na Dezdery Everigist

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post