BENKI YA CRDB YATUMIA MAADHIMISHO YA SIKU YA USHIRIKA DUNIANI 'SUD' KUONESHA FURSA ZA UWEKEZAJI


Benki ya CRDB imeshiriki maadhimisho ya Siku ya Ushirika Duniani (SUD) duniani yaliyofanyika kitaifa mkoani Tabora katika Viwanja vya Ipuli.

Maadhimisho hayo yaliyoanza tarehe 29 Juni 2024 na kuhitimishwa leo tarehe 6 Julai,2024 yalifunguliwa na Naibu Waziri wa Kilimo Mh. David Silinde na kufungwa na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko.

Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya CRDB ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamisheni ya Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania (TCDC), Abdulmajid Nsekela aliungana na wafanyakazi wa Benki ya CRDB kutoka Makao Makuu wakiongozwa na Mkuu wa Kitengo cha Kilimo Biashara, Maregesi Shaaban, pamoja na wafanyakazi wa Kanda ya Magharibi wakiongozwa na Meneja wa Kanda hiyo, Jumanne Wagana.

Benki ya CRDB ikiwa ni mdau mkubwa wa sekta ya ushirika nchini, Benki ambayo pia ndio mdhamini mkuu  imetumia maadhimisho hayo kuonesha fursa za uwezeshaji zinazotolewa kwa wateja wake waliopo kwenye mnyororo wa thamani katika sekta za kilimo, uvuvi, ufugaji, viwanda na usafirishaji.

#CRDBBank
#UlipoTupo




Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post