MWENYEKITI WA UWT TAIFA AONGOZA KONGAMANO LA MAFUNZO YA MATOKEO YA SENSA KWA MAKUNDI MBALIMBALI LILILOANDALIWA NA MBUNGE SANTIEL KIRUMBA SHINYANGA


Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha Mapinduzi Taifa Comrade Marry Pius Chatanda  ameongoza Kongamano la Mafunzo ya Matokeo ya Sensa kwa Makundi mbalimbali lililoandaliwa na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Shinyanga Mhe. Santiel Kirumba lililofanyika Wilayani Kahama Mkoa wa Shinyanga kwa lengo la kutoa Mwelekeo wa CCM kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi 
Mwenyekiti wa Umoja wa wanawake Tanzania UWT, Ndg Mary Chatanda akiwa ameambatana na Wajumbe wa Kamati ya Utekelezaji UWT Taifa, Tarehe 01.06.2024 amefungua Mafunzo ya usambazaji wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya watu na Makazi ya Mwaka 2022 Kwa viongozi na watendaji wa Makundi maalum Wilaya ya Kahama Mkoani Shinyanga

Kongamano hilo liliandaliwa na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Santiel Kirumba lililofanyika Wilayani Kahama Mkoa wa Shinyanga kwa lengo la kutoa Mwelekeo wa CCM kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi mkuu.

Mhe. Mary Chatanda amefikisha salamu za Rais Samia Suluhu Hassan kwa wana Shinyanga kuwa anawapenda sana na kusema kuwa wahakikishe katika chaguzi zijazo Chama Cha Mapinduzi kinashinda kwa kishindo kwani kazi za maendeleo zimefanyika

Mhe. Chatanda ametumia hadhira hiyo kuhimiza Wanawake wenye uwezo na sifa za uongozi kujitokeza kuwania uongozi Katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa Kufanyika Novemba 2024 ili kujaza nafasi za Mwenyekiti wa Mtaa, Kijiji na vitongoji na wajumbe wao.

Kadharika, Mhe. Chatanda amewakumbusha Wanawake na Wananchi kujitokeza Julai 20.2024 kujiandikisha kwenye daftari la Makazi pamoja na Mpiga Kura ili kujiandaa vyema kushiriki katika uchaguzi wa serikali za Mtaa na Uchaguzi Mkuu 2025.

Mbunge Santiel amesema kuwa Kongamano hilo limejumuisha viongozi wa CCM na Serikali wakiwemo Wakurungezi wote wa Halmashauri (Shinyanga), Wabunge, Watendaji, Mama Lishe, Wajasiriamali, Waponda Kokoto, Walimu, Manesi, Maaskari, Watu wenye ulemavu.

Aidha, Mhe. Santiel Eric Kirumba amempongeza na  amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutenga fedha za kuwezesha kufanya Sensa ya watu na makazi.

Vilevile, Mbunge Santiel Eric Kirumba amempongeza Mama Albina Chuwa, Mkurugenzi Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) na kuhakisha wanapata taarifa ya Sensa ya watu na makazi 2022/2023, ili kusaidia kupanga Maendeleo kwa pamoja.

Mhe. Santiel Eric Kirumba ameishukuru Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) kwa kumpa ushirikiano wa kutosha kwani Mafunzo hayo yametolewa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) ikishirikiana na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Shinyanga ambaye ni Santiel Eric Kirumba.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post