ZAMDA SHABANI ASHINDA UCHAGUZI WA NAIBU MEYA MANISPAA YA SHINYANGA KWA 100%

Diwani wa kata ya Ndala Mhe. Zamda Shabani 

Na Shinyanga MC

Diwani wa kata ya Ndala Mhe. Zamda Shabani ameshinda uchaguzi wa naibu Meya Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga uliofanyika katika ukumbi wa Lewis Kalinjuna uliopo ofisi ya Mkurugenzi wa halmashuri ya Manispaa ya Shinyanga ikiwa ni awamu ya pili mfululizo (2023/2024-2024-2025.)

Awali akitoa ufafanuzi juu ya Mgombea nafasi ya Naibu Meya Mkuu wa Division ya Utawala na Usimamizi Rasilimali watu manispaa ya Shinyanga Ndg, Pius Sayayi amesema Halmashauri ya manispaa ya Shinyanga. Mhe Pius Sayayi amesema Halmashauri ilipokea jina moja tu la Mgombea ngazi ya Naibu Meya wa Manispaa, hivyo kwa mujibu wa Sheria za Uchaguzi jina hilo litapigiwa kura za "Ndiyo" na "Hapana"


"Kwa mujibu wa sheria ya Uchaguzi endapo mgombea nafasi husika atakuwa mmoja tu wajumbe watapiga kura za NDIYO au HAPANA ambapo mgombea huyo akifikia asilimia hamsini 50% atakuwa ameshinda Uchaguzi huo", amesema NduguSayayi Mkuu wa Division ya Utawala na Usimamizi Rasilimali watu manispaa ya Shinyanga.


Akitangaza matokeo ya Uchaguzi huo Mwenyekiti wa Uchaguzi ambaye pia ni katibu tawala wa wilaya ya Shinyanga Said Kitinga amesema Ndugu Zamda shabani ameshinda uchaguzi huo kwa asilimia zote


"Jumla ya wapigakura ni 19, kura zilizopigwa ni 19, kura za ndio ni (0) kuta zilizo haribika ni (0) kura za ndio ni (19), hivyo kwa mamlaka niliyopewa Ndugu Zamda Shabani namtangaza kuwa ndiye Mshindi wa ngazi ya Naibu Meya manispaa ya Shinyanga", amesema Ndg Said Kitinga Katibu tawala wilaya ya Shinyanga.

Sambamba na hayo Umefanyika uchaguzi wa kamati za kudumu kwa mwaka 2024/2025 ambapo Mhe, Ezekiel Sabo ameshinda ngazi ya Mwenyekiti wa kamati ya Afya, Elimu na uchumi, Mhe, Hassan Mwendapole ameshinda kuwa Mwenyekiti wa kamati ya Maadili,
Mhe, Elias Andrea Kashinga kuwa Mwenyekiti kamati ya Mipangomiji na Mazingira.

Baada ya Uchaguzi huo Naibu Meya Manispaa ya Shinyana Zamda Shabani amewashukuru wajumbe kwa kumuamini tena kumchagua nafasi hiyo kwa mwaka wa pili Mfululizo.


"Niwashukuru sana waheshimiwa madiwani kwa kuniamini kunichagua tena ili kuendelea kudumu katika nafasi hii ilikuwa si rahisi kwa sababu wote tunaweza lakini mimi ndiye mmeniamini zaidi, ninachoomba kwenu ni ushirikiano. Nitaendelea kukusaidia Mstahiki Meya wakati wowote utakaponihitaji kukusaidia lakini pia nitatoa ushirikiano kwa watu wote ili tuweze kuijenga manispaa yetu". amesema Mhe. Zamda Naibu Meya.


Naye Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM wilaya ya Shinyanga Ndg. Anord Makombe amewataka viongozi wote waliochaguliwa na waheshimiwa Madiwani kutimiza majukumu yao.

"Viongozi wote mliochaguliwa leo mmeaminiwa na Waheshimiwa Madiwani sio kwamba ninyi ni bora sana kuliko hawa wengine ila wamewaamini kuwaongoza, sasa nendeni mkatimize wajibu wenu fanyeni kazi tuondoe tofauti zetu sisi ni wamoja", amesema Ndg. Makombe Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi. CCM Wilaya ya Shinyanga.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post