DAWASA KUUNGANISHA HUDUMA YA MAJISAFI KWA WATEJA ZAIDI YA 200 TEGETA

 


Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es salaam (DAWASA) imeendelea na zoezi la ugawaji wa vifaa vya maunganisho mapya kwa wateja zaidi ya 200 katika mitaa mbalimbali ya Tegeta ikiwemo Wazo, Salasala, Kunduchi, Mbweni na Boko walioomba na kulipia kupata huduma hiyo.

Akizungumza zoezi hilo Meneja wa Mkoa wa kihuduma DAWASA - Tegeta ndugu, Victoria Masele amewashukuru wateja wote kwakua wavumilivu mpaka muda huu ambao sasa wanaenda kuungwa na huduma ya majisafi.

"Niwashukuru wateja kwakuvumilia kipindi chote walipokua wakisubiri kupatiwa vifaa hivi, wateja hawa 200 wote tunaenda kuwaunga na huduma ya majisafi kwa kipindi kifupi sana Ili waanze kufurahia huduma kutoka DAWASA" ameeleza ndugu, Masele.

Ndugu Masele ametoa wito kwa wananchi ambao waliofanya maombi na wamekwishapatiwa kumbukumbu namba kwajili ya kufanya malipo basi waweze kukamilisha zoezi la ulipaji Ili na wao wapate huduma.

Kwa upande wake ndugu, Hillary Kimambo mkazi wa Mbweni ameishukuru DAWASA kwakuwapatia vifaa hivi kwani wanaenda kupata huduma ya majisafi na kuondokana na changamoto ya kununua maji kwa gharama kubwa huku muda mwingi wakiwa hawana uhakika na usalama wa maji hayo Kitendo ambacho kilihatarisha afya zao.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post