DMI KUSAJILI WANAFUNZI BURE PASIPO MALIPO


Chuo Cha Bahari Dar ES Salaam (DMI) kinaendelea na huduma ya usajili wa wanafunzi katika viwanja vya Sabasaba Dar es Salaam bila malipo.

DMI ni moja ya taasisi zilizopo katika maonesho ya 48 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea katika viwanja vya Sabasaba jijini Dar es Salaam.

Timu ya wataalam kutoka chuo Cha Bahari Dar es Salaam -DMI wanaendelea kutoa elimu ya masuala ya ubaharia pamoja na fursa zinazopatikana baharini.

Aidha chuo Cha Bahari Dar es Salaam -DMI kinawakaribisha wananchi kutembelea kwenye Banda lao lililopo ndani ya KARUME HALL.

Huduma mbalimbali zinatolewa ikiwa ni pamoja na usajili wa wanafunzi wanaojiunga na Kozi za Cheti na Diploma bila malipo yoyote pamoja na elimu ya Ubaharia.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post