KIMEI AANZA ZIARA JIMBONI


Mbunge wa Jimbo la Vunjo Mheshimiwa Dkt Charles Stephen Kimei akizungumza na wananchi wa vijiji vya Kisangesangeni na Miwaleni kata ya Kahe, Halmashauri ya Wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro hii leo.

Kimei yupo jimboni kuzungumza na wananchi wa Jimbo hilo kusikiliza na kutolea ufafanuzi wa masuala na kero mbalimbali zinazowakabili wananchi.

Katika ziara yake hiyo aliambatana na diwani wa kata ya Kahe Mhe Aloyce Momburi, wajumbe wa kamati ya siasa ya kata wakiongozwa na katibu wa CCM Kata Ndg Melau Laizer, maafisa watendaji kata na vijiji wakiongozwa na Ndg Happy Msuya pamoja na wataalam toka bonde la Mto Pangani.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post