MRADI WA JULIUS NYERERE UTAZALISHA UMEME MARA MBILI YA TULIONAO KWA SASA

Na Mwandishi wetu _ Malunde 1 blog

Naibu Waziri wa Nishati nchini Mheshimiwa Judith Kapinga amesema mradi wa uzalishaji wa nishati ya umeme wa Julius Nyerere unatarajia kuzalisha megawati mara mbili ya umeme uliopo sasa hapa nchini pindi utakapokamilika.

 Waziri Kapinga amesema hayo leo Julai 03, 2024 wakati wa mkutano wa hadhara katika kijiji cha Kidunyashi kata ya Isagehe manispaa ya Kahama ikiwa ni hitimisho la ziara yake ndani ya wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga.


Akizungumza wakati wa mkutano huo Mheshimiwa Kapinga amesema kukamilika kwa mradi wa uzalishaji umeme wa Julius Nyerere utapunguza changamoto ya mgao na kukatika kwa umeme kwenye maeneo mbalimbali.

 

"Serikali inatekeleza miradi mingi sana kwenye sekta nishati ya umeme ambazo ni uzalishaji, usafirishaji na usambazaji, ndiyo maana iliamua kutenga takribani shilingi Tilioni 6 kwaajili ya ujenzi wa mradi wa uzalishaji umeme wa Julius Nyerere ili kuhakikisha wananchi wanaendelea kupata umeme wa uhakika na pindi utakapokamilika utaweza kuzalisha megawati za kutosha ambazo ni mara mbili ya umeme tuliona kwa sasa", amesema Mheshimiwa Kapinga.


"Lakini pia ipo miradi ya usambazaji na kutanua mtandao wa umeme kwenye vijiji mbalimbali ambapo kupitia wakandarasi wanaosimamiwa na Wakala wa Nishati Vijijini REA kuhakikisha kila kijiji na kitongoji kinafikiwa na huduma ya umeme, suala la umeme kwenye serikali yetu ni kipaumbele chetu", ameongeza Mheshimiwa Kapinga.


Awali akieleza hali ya upatikanaji wa umeme kwenye kata ya Isagehe Diwani wa kata hiyo amesema mpaka sasa kati ya vijiji 24 vijiji 8 ndiyo vimefikiwa na huduma ya umeme vitongoji 8 bado havijafikiwa na huduma hiyo hivyo wamemuomba mkandarasi kuongeza kasi.

 

Kwa upande wake Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Wakili Julius Mtatiro ambaye pia ni mkuu wa wilaya ya Shinyanga amewasihi wananchi kuendelea kuwa wavumilivu wakati serikali ikiendelea kutekeleza miradi yenye manufaa kwa wananchi wake.

Naibu Waziri wa Nishati Nchini Mheshimiwa Judith Kapinga akizungumza wakati wa ziara yake ndani ya Manispaa ya Kahama.

Baadhi ya wananchi waliojitokeza kwenye mkutano huo.

Naibu Waziri wa Nishati Nchini Mheshimiwa Judith Kapinga akizungumza wakati wa ziara yake ndani ya Manispaa ya Kahama.

Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga ambaye pia ni mkuu wa wilaya ya Shinyanga Julius Mtatiro akizungumza wakati wa ziara hiyo ndani ya manispaa ya Kahama.

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Kahama Mhe. Thomas Muyonga akizungumza wakati wa ziara hiyo.


Mmoja wa wananchi akiwasilisha hoja na changamoto wakati wa mkutano huo.
Mwakilishi wa Mkurugenzi mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini REA ambaye pia ni Msimamizi wa Miradi Mhandisi Romanus Lwena akizungumza wakati wa ziara hiyo.

Mkandarasi kutoka Kampuni ya Tontan Project Technology Co. Ltd Jv Group Six International akizungumza wakati wa ziara hiyo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post