TBS KANDA YA MASHARIKI YATEKETEZA TANI 4.5 ZA BIDHAA HAFIFU


NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS), Kanda ya Mashariki limeteketeza bidhaa hafifu tani 4.5 zenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 90 mara baada ya kufanya ukaguzi na kufanikiwa kukamata bidhaa hizo.

Akizungumza wakati wa zoezi hilo ambalo limefanyika leo Julai 5,2024 Pugu Jijini Dar es Salaam, Kaimu Meneja Kanda ya Mashariki, Francis Mapunda amesema kuwa walifanya oparesheni ya Ukaguzi Kanda ya Mashariki na kubaini kuwepo udanganyifu kwa baadhi ya wafanyabiashara kuuza bidhaa zilizo chini ya kiwango.

Amesema kuwa bidhaa hizo wamezikamata katika Mkoa wa Dar es Salaam, Morogoro na Pwani ambapo bidhaa hizo zilikuwa hazijasajiliwa, zilizoisha muda wa matumizi pamoja na bidhaa zisizosalama kwa walaji.

Aidha amewaonya wafanyabiashara wanaouza bidhaa zilizoisha muda wake ambapo amesema wanapaswa kuwa na utamaduni wa kukagua bidhaa zao na kama zimeisha muda wake ni vyema wakaziondoa mara moja ili kuepusha changamoto zinazoweza kujitokeza.

Pamoja na hayo amewaasa wananchi kuwa makini na ununuaji wa bidhaa sokoni ikiwemo chakula kuangalia tarehe ya za kutengenezwa na tarehe za kuisha muda wake lakini vilevile na kuangalia kwenye mitandao ya kijamii bidhaa ambazo zimepigwa marufuku kwamba si salama kwa matumizi ya binadamu.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post