WANAHARAKATI WAIPONGEZA SERIKALI KWA MAFANIKIO DIRA YA TAIFA 2025


WANAHARAKATI wa masuala ya Jinsia na Maendeleo wameipongeza Serikali kwa uwajibikaji mkubwa kwenye Dira ya taifa ya miaka 25 iliyopita katika nyanja ya elimu ,afya pamoja na sekta ya habari na mawasiliano.

Pongezi hizo zimetolewa leo Julai 10,2024 Mabibo -Jijini Dar es salaam,kwenye semina za Jinsia na Maendeleo (GDSS) zinazofanyika kila jumatano TGNP-Mtandao,

Akizungumza wakati katika semina hiyo, Mdau wa Jinsia na Maendeleo Mwl.Vivian Ugurumo amesema elimu bure kwa wote, ujenzi wa madaraja, zahanati kila kata pamoja na barabara ni mafanikio kwa miaka 25 iliyopita ambapo awali havikuwepo vyote vilivyofanyika.

"Kuna masuala kama jamii tunaona tumefanikiwa sasa hivi tunaona watoto wanasoma kuanzia shule ya msingi hadi vyuo,tunaona mabinti nao wanasoma, kumekuwa na redio za mtandaoni,televisheni za mtandaoni ambapo kipindi hicho hazikuwepo"Amesema.

Aidha Vivian ameeleza kuwa katika kipindi cha miaka 25 iliyopita ya dira ya taifa kwenye nyanja ya afya maboresho makubwa yamefanyika kwa kuingizwa vifaa vya kisasa kwenye matibabu pamoja na upatikanaji rahisi wa dawa.

Amesema kwenye sekta ya afya huduma kwa wazee pamoja na huduma ya mama na mtoto bado ni changamoto kwani bado kuna malalamiko kwamba wanalipishwa kwa ajili ya kupata matibabu.

Pamoja na hayo Vivian ameomba Dira ijayo kila sekta iingize masuala ya mlengo wa kijinsia pamoja na makundi yote,bila kuwaacha nyuma walemavu kwa aina zake.

Kwa upande wake, Mwanaharakati wa masuala ya Jinsia,Jasmine Mohamed amesema mafanikio yaliyooatika kwa miaka 25 ni makubwa ambapo amegusia suala la miundombinu ya maji ya Sasa ukilinganisha na miaka 25 iliyopita kunatofauti kubwa ingawa bado kuna changamoto ammbazo zinatakiwa kufanyiwa ufumbuzi.

Aidha Jasmine ameshauri yafanyike maboresho katika dira mpya inayokuja kwa kuongeza idadi ya walimu mashuleni pamoja na kusimamia vyema miundombinu iliyoanzishwa kwa upande wa maji na usafirishaji.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post